Rais Samia azindua Kiwanda cha Sukari Mkulazi, ahimiza ushirikiano na sekta binafsi

HomeKitaifa

Rais Samia azindua Kiwanda cha Sukari Mkulazi, ahimiza ushirikiano na sekta binafsi

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameendelea kutekeleza ahadi zake kwa vitendo baada ya kuzindua Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi kilichopo mkoani Morogoro. Kiwanda hiki kinachozalisha tani 200-250 za sukari kwa siku, kinatarajiwa kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza upungufu wa sukari nchini, huku pia kikitoa ajira kwa Watanzania zaidi ya 5,000.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa kiwanda cha Sukari Mkulazi, Mbigiri mkoani Morogoro, tarehe 7 Agosti, 2024.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais Samia alisisitiza umuhimu wa sekta binafsi kushirikiana na serikali katika kuwekeza ndani ya nchi na kuingia kwenye miradi ya pamoja. “Sekta binafsi iwekeze ndani ya nchi, waingie kwenye miradi pamoja na serikali,” alisema.

Sehemu ya kiwanda cha Sukari Mkulazi ambapo miwa hupokelewa na kuchakatwa katika hatua za awali, ambacho kimezinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mbigiri mkoani Morogoro, tarehe 7 Agosti 2024.

Pia, aliwapongeza wale wote waliowezesha kutengeneza ajira kupitia kiwanda hicho na kuwatakia mafanikio mema katika kuendesha mradi huo kwa manufaa ya taifa. Rais Samia aliendelea kusisitiza dhamira yake ya kuendeleza miradi yote iliyozinduliwa na watangulizi wake, akionyesha kwamba uzinduzi wa kiwanda hiki ni uthibitisho wa ahadi hizo.

error: Content is protected !!