Jeshi la Polisi la Tanzania limetangaza nafasi za ajira kwa vijana wa Kitanzania wenye sifa stahiki, likiwataka kutuma maombi yao kupitia mfumo wa ajira wa jeshi hilo kabla ya tarehe 04 Aprili, 2025.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali (IGP) Camillus Wambura Machi 20, 2025 nafasi hizo zinahusisha waombaji wenye elimu ya kidato cha nne, kidato cha sita na wahitimu wa shahada, stashahada na astashahada katika taaluma mbalimbali.
TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA JESHI LA POLISIhttps://t.co/NRMdsPNLRM pic.twitter.com/ylIyXBWQEG
— Police Force TZ (@tanpol) March 21, 2025
Miongoni mwa vigezo vilivyotajwa kwa waombaji ni kuwa na uraia wa Tanzania kwa kuzaliwa, afya njema kimwili na kiakili iliyothibitishwa na daktari, kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu, kutokuwa na alama za kuchorwa mwilini (tatoo), na kutowahi kutumia madawa ya kulevya ya aina yeyote.