Ofisa wa Tume aliyepotea Kenya akutwa amefariki Kilombero

HomeKimataifa

Ofisa wa Tume aliyepotea Kenya akutwa amefariki Kilombero

Saa chache baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya Kenya kumtangaze Dk William Ruto kuwa Rais mteule wa Kenya, mwili wa ofisa wa tume hiyo aliyepotea akiwa kituo cha kupigia kura umepatikana katika msitu wa Kilombero akiwa amefariki.

Ofisa huyo Daniel Musyoka (53), alikuwa msimamizi wa Kaunti ya Embakasi Mashariki iliyopo katika jiji la Nairobi na mwili wake umepatikana jana, Jumatatu Agosti 15, 2022 katika msitu eneo la Kajiado.

Akizungumzia kupatikana kwa mwili huo, Ofisa wa Polisi wa Loitoktok, Kipruto Ruto, amesema walipewa taarifa za kuwapo kwa mwili huo ambao baadaye dada zake waliutambua mwili huo ni wa ndugu yao.

error: Content is protected !!