Babalevo ashutumiwa kwa utapeli wa milioni 12

HomeBurudani

Babalevo ashutumiwa kwa utapeli wa milioni 12

Aliyekuwa msanii wa Baba Levo mwanadada Oti ameeleza jinsi alivyotapeliwa kiasi cha milioni 12, kupigwa pamoja na kuachwa kwenye mataa na msanii huyo baada ya kusaini mkataba wakumsimamia katika kazi zake za muziki.

Akizungumza kwenye mahojiano na Bongo 5, Oti ameeleza kwamba Baba Levo alimuahidi kumsimamia kazi zake za muziki na kumfanya kuwa msanii mkubwa kwa kufanya colabo na wasanii wakubwa kama Zuchu na Rayvanny huku akimtumia hela nyingi lakini hakuna kilichofanyika na baadaye kumtelekeza.

“Ilifika wakati akawa ananiambia Oti inatakiwa tufanye kolabo na Zuchu, tufanye kolabo na Rayvanny, namtumia hela anakula, kwahiyo hivi vitu vinafika wakati vinaniuma unamuachaje mtu ambaye umemuharibia kila kitu,” amesema Oti.

Oti amesema anaenda kumfungulia kesi Baba Levo amlipie pesa hizo na kesi yakumpiga mbele ya watu akiwa studio huku akimtaja Bob Junior kama mmoja wa watu walioshuhudia tukio hilo la kupigwa.

error: Content is protected !!