Tanzania kinara kwa uhuru wa vyombo vya habari Afrika Mashariki

HomeKimataifa

Tanzania kinara kwa uhuru wa vyombo vya habari Afrika Mashariki

Tanzania imekuwa nchi bora yenye uhuru wa vyombo vya habari katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya maboresho yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan yaliyoleta mageuzi makubwa.

Ripoti ya Reporters Without Boarders (RWB) inaonyesha kwamba Tanzania imepanda viwango kutoka nafasi ya 143 hadi nafasi ya 97 mwaka 2024.

Kupanda kwa viwango kunatokana na hatua zilizochukuliwa na Rais Samia za kubadilisha mwelekeo wa nchi ndani ya miaka yake mitatu ya uongozi na kuondoa vizuizi vya uhuru wa habari vilivyokuwepo.

Baadhi ya mabadiliko yaliyofanyika ni pamoja na kufungulia na kuviachia huru vyombo vya habari vilivyofungwa, mabadiliko ya Sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari 2016 na Kanuni za Sheria ya Mawasiliano ya Kieletroniki na Posta (EPOCA) 2010.

Uhuru wa Vyombo vya Habari ya Dunia ya Mwaka 2024:

Tanzania – 97

Kenya – 102

Burundi – 108

DR Congo – 123

Uganda – 128

Sudan Kusini – 136

Rwanda – 144

Somalia – 145

error: Content is protected !!