Askari 300 kuwasaka Panya Road

HomeKitaifa

Askari 300 kuwasaka Panya Road

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema wametoa askari 300, kwa ajili ya kuendesha opereseheni ya kuwakamata Panya Road, ambao wamekuwa wakifanya mauaji na kujeruhi wakazi wa mkoa huo.

Amesema mzazi na mlezi atakayepotelewa na kijana wake kwa wakati huu, atatakiwa kwenda kumtafuta hospitalini au kwenye vituo vya polisi.

Makalla ameyasema hayo leo Septemba 15, wakati wa ziara yake katika Kata ya Zingiziwa Chanika, Dar es Salaam.

“Hatutacheka nao tena, kwani walianza hapa Zingiziwa, Tabata Kinyerezi na sasa Mzimuni Kawe, tutatimiza wajibu wetu na mzazi utakayetaka kumuwekea dhamana mtoto wako, ujipange kwani tutaanza na wewe,” amesema Makalla

error: Content is protected !!