Hizi hapa sifa 13 za iPhone 13

HomeKimataifa

Hizi hapa sifa 13 za iPhone 13

 

– Ina umbo jembamba ambalo utafiti unaonesha watu wengi wanapenda simu nyembemba kwa sasa.

– Kioo chake kina teknolojia mpya aina ya ‘Ceramic’ ambapo ndio itakuwa simu yenye kioo imara zaidi kuliko simu nyingine dhidi ya kuanguka na kuchubuka.

– Iphone 13 kioo chake hakiruhusu maji na umbile lake kwa pembeni limewambwa kwa aluminiam.

–  Unaweza kupata  iPhone 13 kati rangi 5 tofauti, ambazo ni nyekundu,  pinki, bluu, nyeusi  na nyeupe.

– Ili kulinda mazingira, “material” kutoka kwenye chupa cha plastiki zilizorejeleshwa (recycled bottles) ni miongoni mwa “material” yalizotumika kuunda umbo la nje la iPhone 13

– Apple wametoa matoleo manne ya iPhone 13 ambayo ni iPhone 13, iPhone 13 Mini, iPhone 13 Pro na iPhone 13 Pro Max ambapo zote zina tabia za kufanana.

– Zaidi ya asilimia 90% ya umbo la iPhone 13 limeigwa kutoka kwa iPhone 12. Hivyo kwa kuzitazama hakuna tofauti kubwa.

– Uwezo wa betri kukaa na chaji umeongezwa, kutoka saa moja na nusu mpaka saa mbili kwa nusu kama utatumia mfululizo.

– iPhone 13 imeboreshwa Camera zaidi. Inaweza kupiga picha pana zaidi (ultra wide lens), na yenye mwanga mzuri hata katika eneo lenye mwanga mdogo.

– iPhone 13 imewekewa uwezo wa kasi ya 5G kwenye kuperuzi.

– iPhone 13 imewekewa uwezo wa ‘Cinematic Mode’. Yaani imepewa uwezo kama Camera zinazotumika kwenye kurekodi filamu.

– Unaweza kupiga picha/video ukaihariri (edit) hapo hapo na kuituma bila kupungua ubora. Inauwezo wa kuhamisha ‘focus’, yaani kufanya akili na macho yako kuhama kulingana na uelekeo wa camera katika picha.

– Super Retina XDR Display, inafanya iPhone 13 kuwa simu yenye kasi zaidi katika kuchakata mafaili, kutafuta na muonekano mzuri zaidi.

error: Content is protected !!