Kijana aliyeokoa watu kwenye ndege ya Precision Air apewa milioni 1

HomeKimataifa

Kijana aliyeokoa watu kwenye ndege ya Precision Air apewa milioni 1

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila amemkabidhi kijana mmoja mvuvi aliyejitosa kwenye maji akijaribu kuwaokoa wahanga wa ajali ya ndege ya Precison Air, kiasi cha shilingi milioni moja zilizotolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kama pongezi kwa kitendo hicho cha kishujaa.

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya marehemu waliopata ajali hiyo katika Uwanja wa Kaitaba, Chalamila alisema kwa ujasiri mkubwa alioonyesha kijana huyo serikali ya mkoa wa Kagera wamepanga pia kumpa pongezi.

Pia, Chalamila alimuomba Waziri Mkuu kutoa fedha kidogo kwenye mfuko wa mahafa kwa ajili ya kuwapa mafunzo ya uokoaji wavuvi wanaofanya kazi zao kando ya Ziwa Victoria.

 

error: Content is protected !!