LNG kunufaisha wananchi wa Lindi na Mtwara kimiundombinu

HomeKitaifa

LNG kunufaisha wananchi wa Lindi na Mtwara kimiundombinu

Rais Samia Suluhu Hassan amesema barabara na miundombinu yote ambayo itahusika na mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) mkoani Lindi itaanza kujengwa utekelezaji wa mradi huo utakapoanza.

Rais amesema hayo leo wakati akionge na wananchi wa kata ya Nanguruwe, Mtwara Vijijini mkoani Mtwara.

“Lindi na Mtwara tunatarajia mradi mkubwa sana wa gesi, ule mradi utakapokuja barabara zote zinazohusiana na mradi ule zinakwenda kujengwa.” amesema.

Rais amesema kwa sasa serikali ipo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo ili mradi wa LNG uanze kujengwa.

Raisi Samia Suluhu Hassan yupo Mtwara kwa ziara ya siku nne kukagua miradi ya maendeleo, kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

error: Content is protected !!