Mguu uliokatwa wa maiti mwenye ualbino wapatikana

HomeKitaifa

Mguu uliokatwa wa maiti mwenye ualbino wapatikana

Zikiwa tayari zimepita wiki mbili tangu kufukuliwa kwa kaburi la Shekigenda Kijangwa (35) mwenye ulemavu wa ngozi (ualbino) na kukutwa na mguu wake umenyofolewa na kuchukuliwa, Jeshi la Polisi limeupata.

Kaburi hilo limefukuliwa oktoba 24 mwaka huu, katika kijiji cha Tanda Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli. Akizungumza na wanahabari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Sofia Jongo alisema baada ya tukio hilo polisi walifanya msako na walifanikiwa kukamata watu watatu walioonyesha mguu huo.”

> Watatu washikiliwa kufukua kaburi la Albino

Mguu huo ulikuwa umefukiwa kwenye shamba la mmoja wa wahutumiwa hao lililopo umbali wa kilomita 30 kutoka alipozikwa marehemu” alisema kamanda Jongo.Kama Jongo alimazilia kuwa kusema kuwa watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi wa tukio hilo kukamilika.

error: Content is protected !!