Mke auliwa na mchepuko wake

HomeKimataifa

Mke auliwa na mchepuko wake

Mwili wa mwanamke aliyetambulika kwa jina la Teddy Mallya mkazi wa Ilboru Kisiwani, Arumeru mkoani Arusha umekutwa umetupwa kwenye shamba la migomba akiwa mtupu na baadhi ya majeraha mwilini ikiwemo ya kung’atwa na meno huku akidaiwa kuuawa na hawara yake (mchepuko).

Mwili huo ulipatikana jana majira ya saa 2:30 asubuhi baada ya wapita njia kuuona na kutoa taarifa, Taarifa za wakazi wa eneo hilo wanadai kuwa marehemu alikua na uhusiano wa siri na mwanaume nje ya ndoa ambaye anadaiwa kutekeleza mauaji hayo kutokana na kumtuhumu marehemu kuwa alitoa ujauzito wake.

Mume wa marehemu, Richard Lanyuni alisema mkewe alikuwa mfanyabiashara wa pombe za kienyeji aina ya mbege , hakuonekana kurejea nyumbani muda wa kawaida na ilipotimu majira ya saa saba usiku niliamua kulala ndipo kesho yake alipata taarifa za kuuawa.

“Kuhusu mke wangu kuwa na uhusiano na mwanaume huyo siwezi kujua ila hakuwa na ujauzito. Naomba vipimo vya kitaalamu vifanyike kujua kama kweli alikuwa na ujauzito maana ana shughuli zake mimi siwezi kumchunguza sana” alisema Richard

Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justin Masejo alisema jeshi linamshikilia mwanaume mmoja kwa tuhuma za kumuua mwanamke huyo, na kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wamtaa wa Ilkiroriki, Emmanuel Lazaro, mtuhumiwa anadaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu na alikamatwa kutokana na baadhi ya nguo zake na viatu kukutwa eneo la tukio.

error: Content is protected !!