Polepole aondolewa hadhi ya ubalozi, uteuzi wake watenguliwa

HomeKitaifa

Polepole aondolewa hadhi ya ubalozi, uteuzi wake watenguliwa

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kuwa Rais Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Hamphrey Polepole aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, na pia kumuondolea hadhi ya ubalozi.
 
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dk. Samwel Shelukindo, kufuatia barua rasmi kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, ikieleza kuwa uamuzi huo umefanywa kwa mamlaka aliyopewa Rais chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Aidha, kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma, Rais Samia amemuachisha kazi Hamphrey Polepole kwa msingi wa manufaa ya umma.
 
Uamuzi huo umeanza kutekelezwa rasmi kuanzia Julai 16, 2025.
error: Content is protected !!