Wafanyakazi kuongezewa mshahara

HomeKitaifa

Wafanyakazi kuongezewa mshahara

Rais Samia Suluhu Hassan ameahidi wafanyakazi kuwa lile Jambo aliloahidi Mei Mosi mwaka jana pale Mwanza la kuwaongeza mshahara linatekelezwa.

Amesema hayo wakati wa hafla za maadhimisho Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi), Dodoma -Tanzania na kuongeza kuwa serikali itaendelea kupunguza kodi kama ilivyofanya mwaka huu lakini pia itaongeza mshahara wa wafanyakazi japo si kwa kiwango kikubwa.

“Ndugu zangu, jambo letu lipo si kwa kiwango kilichosemwa na TUCTA kwasababu mnajua hali ya uchumi wetu na hali ya uchumi wa dunia. Kwasababu nilishatoa ahadi mwaka jana, kwahiyo nimeagiza jambo liwepo, mahesabu yanaendelea tutajua lipo kwa kiasi gani,” amesisitiza Rais Samia.

Pia, Rais amewaonya wale wote wanaopandisha bei za bidhaa kiholela na panya road wanaohatarisha maisha ya wananchi wengine kuhakikisha wanaacha mara moja tabia hiyo.

error: Content is protected !!