Wanaotumia iPhone hizi hatarini kuikosa Whatsapp

HomeKimataifa

Wanaotumia iPhone hizi hatarini kuikosa Whatsapp

Kampuni ya Facebook, inayomiliki mtandao wa WhatasApp, imetangaza kuwa inaboresha mfumo wa programu tumishi wa WhatsApp hivyo kuwataka watumiaji wa baadhi ya simu za iPhone kufanya maboresho (updates) ya WhatsApp zao ili kuendana na mabadiliko hayo.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Guardian la Uingereza, Apple imesema mchakato wa WhatsApp kuacha kutumika kwenye baadhi ya iPhone utaanza Novemba 1 2021, hivyo kila mmoja aboreshe WhatsApp yake mapema kuepuka kadhia.

Apple imetangaza kuwa iPhones zote zilizotoka nyuma ya mwaka 2016 zitakumbwa na kadhia hiyo, na baadhi ya mbele ya 2016, hivyo watu wanapaswa kuboresha WhatsApp zao angalau kwenye mfumo wa iOS 10.

Zifuatozo ni iPhone ambazo zinapaswa kuboreshwa ili kuendelea kutumia WhatsApp.

  1. iPhone 5
  2. iPhone 5C
  3. iPhone 5S
  4. iPhone 6
  5. iPhone 6 Plus
  6. iPhone SE (1st-gen)
  7. iPhone 6S
  8. iPhone 6S Plus
  9. iPhone 7
  10. iPhone 7 Plus
  11. iPhone 8
  12. iPhone 8 Plus
  13. iPhone X
  14. iPhone XR
  15. iPhone XS
  16. iPhone XS Max
  17. iPhone 11
  18. iPhone 11 Pro
  19. iPhone 11 Pro Max
  20. iPhone SE (2nd-gen)
error: Content is protected !!