Waziri Mkuu aenda Korea Kusini ziara ya siku tatu

HomeKitaifa

Waziri Mkuu aenda Korea Kusini ziara ya siku tatu

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameondoka nchini kwenda Seoul, Jamhuri ya Korea kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.

Taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu ilieleza kuwa akiwa Korea Kusini, Majaliwa atakutana na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Han Duck-soo.

“Pia anatarajiwa kushiriki kongamano la biashara na kukutana na wamiliki wa makampuni makubwa na wenye viwanda.Vilevile, atakuna na Watanzania waishio Korea Kusini,” ilieleza taarifa hiyo kwa vyombo vya habari.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa kupitia vikao hivyo, Tanzania inatarajiwa kuimarisha uhusiano na KOrea Kusini uliodumu kwa miaka 30.

error: Content is protected !!