Asilimia 84 ya wananchi husikiliza redio

HomeKitaifa

Asilimia 84 ya wananchi husikiliza redio

Ripoti ya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 inaeleza kwamba chombo cha habari kinachotumika zaidi ni redio ambapo 32% ni wanawake na 52% ni wanaume wenye umri wa miaka 15-49 wanasikiliza redio angalau mara moja kwa wiki.

Kwa upande wa televisheni, 30% ya wanawake na 47% ya wanaume wanatazama angalau mara moja kwa wiki, huku 6% ya wanawake na 21% ya wanaume wanasoma magazeti kila wiki.

Aidha, ripoti inaeleza 54% ya wanawake na 34% ya wanaume hawapati huduma hizi tatu za habari angalau mara moja kwa wiki.

error: Content is protected !!