Manufaa 6 nchi inayopata kwa kufanya sensa.

HomeKitaifa

Manufaa 6 nchi inayopata kwa kufanya sensa.

Umuhimu wa sensa upo katika kutoa picha na mwelekeo wa jamii kwa wakati fulani katika mabadiliko mengi na endelevu, ambayo hayawezi kufafanuliwa kupitia njia nyingine bila kukusanya data. Sensa hutoa data zitakazotumika kulinganisha makadirio ya data ya idadi ya watu na huduma za kijamii na kiuchumi.

Sensa kamili ni tofauti na njia zingine za kitakwimu kwa namna zifuatazo:
1. Kuisadia Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia mchakato wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025, mageuzi ya masuala ya afya na jamii, pamoja na ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo za kimataifa;

2. Taarifa za idadi ya watu husaidia katika mamlaka za wilaya katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye uwiano wa mgawanyo wa rasilimali;

3. Taarifa za msingi za hali ya kidemografia, kijamii na kiuchumi za idadi ya watu na makazi za mipango katika ngazi zote;

4. Kigawio katika kukokotoa viashiria vingine mfano Pato la mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa, Ajira na ukosefu wa Ajira na kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi;

5. Taarifa itakayowezesha serikali kujua ongezeko la idadi ya watu, kwa mgawanyo na viashiria vingine, ambavyo ni muhimu kwa usimamizi wa mazingira; na

6. Msingi wa utawala bora na ujumuishaji wa demokrasia. Takwimu sahihi za Sensa zinahitajika kwa ajili ya ugawaji wa majimbo ya uchaguzi kwa ufanisi, kurekebisha mipaka ya kiutawala katika serikali za mitaa.

error: Content is protected !!