Misharahara mipya wafanyakazi wa ndani na hotelini

HomeKitaifa

Misharahara mipya wafanyakazi wa ndani na hotelini

Serikali imetangaza viwango vipya vya kima cha chini cha mishahara kwa wafanyakazi wa ndani na hotelini ambavyo vitaanza kutumika Januari 1, 2023.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,  Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako katika tangazo lilitolewa katika Gazeti la Serikali, amesema viwango hivyo ni kwa sekta binafsi.

Viwango hivyo vitawanufaisha zaidi wafanyakazi wa kazi za ndani wale wasioajiriwa na wanadiplomasia, wafanyabiashara wakubwa na maafisa wenye stahiki ambapo watakuwa wanalipwa Sh60,000 kwa mwezi kuanzia mwaka ujao.

Kiwango hicho kimeongezeka kutoka Sh40,000 waliyokuwa wakilipwa hapo awali kwa mujibu wa Takwimu muhimu za Tanzania za mwaka 2018 zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Wafanyakazi wa ndani wanaoilipwa kima cha chini cha mshahara cha juu kuliko wengine ni wale wafanyakazi wa kazi za ndani walioajiriwa na wanadiplomasia na wafanya biashara wakubwa. Kwa mujibu wa tangazo hilo watalipwa Sh250,000.

Kima cha chini cha mishahara cha wafanyakazi wa majumbani na hotelini

250,000- Wafanyakazi wa kazi za ndani walioajiriwa na wanadiplomasia na wafanyabiashara wakubwa

200,000- Wafanyakazi wa kazi za ndani walioajiriwa na maafisa wenye stahiki

120,000- Wafanyakazi wa kazi za ndani, isipokuwa wale walioajiriwa na wanadiplomasia, wafanyabiashara wakubwa na maafisa wenye stahiki wasioishi katika kaya ya mwajiri

60,000- Wafanyakazi wa kazi za ndani wengine wa nyumbani ambao hawajaanishwa hapo juu

300,000- Hotel kubwa au za kitalii

180,000- Hoteli za kati

150,000- Migahawa , nyumba za kulala wageni na baa

error: Content is protected !!