Rais Samia Suluhu Hassan ametoa msamaha kwa wafungwa elfu nne mia nane themanini na saba (4,887) ambapo arobaini na mbili (42) kati yao wanaachiliwa huru tarehe 26 Aprili, 2025 na elfu nne mia nane arobaini na tano (4,845) wanabaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya kupewa msamaha huu.
Msamaha huo umetolewa leo wakati Taifa likiadhimisha Miaka 61 ya Muungano wa Tanzania.
MSAMAHA WA MHE. RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA WAFUNGWA KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANZANIA pic.twitter.com/sfQHPtXV0j
— WizarayaMamboyaNdani (@WizaraMNN) April 26, 2025