Tanzania kusambaza umeme Afrika

HomeKitaifa

Tanzania kusambaza umeme Afrika

Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 400 kutoka Iringa, Tanzania hadi Zambia (TAZA) utaanza kutekelezwa Januari mwakani na utakamilika Januari 2025, kwa gharama ya Sh trilioni 1.4.

Mrdai huo utawezesha kuimarika kwa upatikanaji wa umeme katika mkoa wa Iringa, Njombe, Mbeya , Songwe na Rukwa pamoja na kuiwezesha Tanzania kufabya biashara ya umeme katika nchi za Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki.

Waziri wa Nishati, January Makamba ameyasema hayo juzi wakati alipotembelea eneo kutakapojengwa kituoc ha kupoza na kukuza umeme cha Tunduma wilayani Momba, Mkoa wa Songwe.

Kituo hicho ni moja kati ya vituo vitano vya kupoza umeme vitakavyojengwa kwenye mradi huo.

error: Content is protected !!