Watu 31 Wafariki wakigombea chakula

HomeKimataifa

Watu 31 Wafariki wakigombea chakula

Takriban watu 31 wamefariki wakati mkanyagano ulipozuka kusini mwa Nigeria wakati wa hafla ya kutoa misaada ya kanisa ambapo chakula kilikuwa kikigawanywa, polisi walisema.

Maafa hayo yalitokea katika mji wa Port Harcourt katika jimbo la Rivers nchini Nigeria, msemaji wa polisi wa eneo hilo Grace Iringe-Koko alisema, na kuthibitisha idadi ya vifo vya watu 31.

Vyombo vya habari vya Nigeria viliripoti tukio lililoandaliwa na kanisa la King’s Assembly lilikuwa likitoa chakula na zawadi kwa maskini katika uwanja wa michezo.

Nigeria imeshuhudia majanga kadhaa ya mkanyagano juu ya usambazaji wa chakula katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na mpango wa chakula wa shirika la misaada kaskazini mwa Jimbo la Borno ambapo wanawake saba walikanyagwa hadi kufa mwaka jana.

 

error: Content is protected !!