Wezi wamuibia Pogba

HomeMichezo

Wezi wamuibia Pogba

Wezi wamemuibia kiungo wa Manchester United, Paul Pogba medali yake ya ushindi wa Kombe la Dunia baada ya kuvunja na kuingia nyumbani kwake na kuiba wakati Manchester United ilipokuwa ikicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid.

Pogba amesema wakati wezi hao wakifanya tukio hilo ndani ya nyumba kulikuwa na watoto wake wawili na dada wa kazi jambo lililompa hofu sana na kueleza nini kilichukuliwa.

“Kulikuwa na vito vya thamani kutoka kwa mama yangu na medali yangu ya ubingwa wa Kombe la Dunia.”

“Hofu yangu kubwa ilikuwa ni kwa watoto wangu wawili waliokuwa nyumbani pamoja na dada wa kazi wakati tukio hilo lilipotokea,” alisema Pogba.

Pogba amekuwa Man United tangu aliporejea katika klabu hiyo wakati huo ikiwa ni rekodi ya dunia ya uhamisho wa Pauni milioni 89(sawa na Sh bilioni 274) akitokea Juventus mwaka 2016.

error: Content is protected !!