Kumbukizi ya siku ya kifo cha Michael Jackson

HomeBurudani

Kumbukizi ya siku ya kifo cha Michael Jackson

Siku kama ya leo Juni 25 mwaka 2009 dunia ilimpoteza nguli wa muziki wa dansi Michael Jackson aliyefariki baada ya kuzidisha kiasi cha dawa wakati akijiandaa na ziara ya tamasha lake la THIS IS IT.

Wakati wa uhai wake, Michael alijinyakulia tuzo nyingi kutokana na kazi zake nzuri za kisanaa alizokuwa akifanya na kukubalika dunia nzima.

Tuzo alizowahi kushinda.
– Grammy Awards 13
– Billboard Awards 86
– American Music Awards (AMA) 26
-Guinnes World Records 13 na muuzaji bora wa albamu katika historia.

Michael alifariki akiwa na umri wa miaka 50 ni kati ya wasanii waliokuwa na vipaji lukuki kama kuimba,kucheza, kutunga, na kuigiza.

error: Content is protected !!